Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Makumbusho ya Taifa la Tanzania

ZANA NA SILAHA ZILIZTUMIKA KIPINDI CHA VITA YA MAJIMAJI

Imewekwa: 20 Dec, 2023
ZANA NA SILAHA ZILIZTUMIKA KIPINDI CHA VITA YA MAJIMAJI

Makumbusho ya Kumbukumbu ya vita vya Majimaji ndiyo makumbusho pekee nchini Tanzania ambayo yanahifadhi na kulinda historia ya vita hiyo na baadhi ya silaha na zana halisi za asili zilizotumika wakati wa Vita vya Majimaji ikiwemo ngao (vikopa,) shoka za vita (vinjenje), vilabu (vibonga), na mikuki (migoha). Pia, baadhi ya picha halisi za wapiganaji walionyongwa tarehe 27 Februari 1906 na maeneo ya historia kama kaburi la halaiki, kaburi la chifu Songea na Eneo lililotumika kunyongea wapiganaji wa vita vya Majimaji mjini Songea.